NOVENA KWA MTAKATIFU ANTONIO WA PADUA
PAROKIA YA MTAKATIFU ANTONIO WA PADUA DCK: JIMBO KATOLIKI NAKURU
3rd – 12th June 2020
JUMATANO: 3rd June: Historia ya Mtakatifu Antonio wa Padua
Mt Anthony wa Padua alizaliwa mwaka 15th Agust 1195 huko Lisbon,Ureno.Aliitwa
Fernando Martins.Alizaliwa katika familia njema yenye uwezo.Akiwa na umri wa miaka
15,aliomba kupelekwa seminari ya Santa Cruz katika mji wa Coimbra,ambako alisoma
teolojia na kilatini.
Akapata daraja la upadre,na akawa hapo hapo mjini Coimbra.Wakaja Wa franciscan ambao
walitengeneza makao yao nje ya mji.Padre Fernando Martin akawapenda,akaomba ruhusa ili
ajiunge nao.Aliporuhusiwa akajiunga nao,akabadili jina,akaitwa Anthony.
Akasafiri mpaka Morocco,kueneza neno la Mungu.Huko akaugua sana,ikabidi arudishwe
Coimbra kwa matibabu.Chombo alichopanda kilivunjika kwa dhoruba,hata hivyo Mtakatifu
Antonio alifika Sicily, na akapelekwa katika mji wa Tuscany ili apate matibabu na
mapumziko.Wakati akiendelea na matibabu,alitumia muda wake mwingi akisali na kusoma.
Muda huo pia walipata wageni ambao walikuwa Wa Dominican. Kukawa na hali ya
kutegemea kila upande kutoa mahubiri. Mkuu wa Wa franciscan alimwambia Mtakatifu
Antonio atoe mahubiri kadiri Roho Mtakatifu atakavyomjaalia. Akatoa mahubiri
yaliyowagusa wote,na kuwasisimua mno.
Habari za mahubiri hayo zikamfikia Mtakatifu Francis wa Assisi,ambaye alipomuona
Mtakatifu Anthony wakawa marafiki. Mt Anthony alikuwa na kitabu cha zaburi,ambacho
ndani yake kulikuwa na mafundisho ya ufafanuzi kwa wanafunzi. Kitabu hicho kwake
kilikuwa kitu chenye thamani mno.Mwanafunzi mmoja aliamua kutoroka seminarini,akaiba
na kitabu hicho.Mt Anthony alisali akiomba kitabu hicho kipatikane na kirudi kwake.Lakini
yule aliyekiiba alirudi nacho,akamrudishia.Kitabu hicho kimehifadhiwa katika kanisa la
Bologna hata sasa.
Mt Anthony aliendelea, kuhubiri na kufundisha katika miji mbalimbali; Ufaransa na Italia.
Kuna wakati aliamua kwenda mtoni, akahubiria samaki baada ya watu kukosa kusikiliza
mahubiri yake.Watu walivyogundua utulivu na usikivu wa samaki nao wakakusanyika na
kusikiliza.
Mt Anthony alifariki mwaka wa 13th June 1231.Akatangazwa Mtakatifu Siku 336 baada ya
kifo chake na Papa Gregory wa IX. Mwaka 1946 Papa Pio wa XII alimtangaza Mtakatifu
Antonio kuwa Daktari wa kanisa.
1
SIKU YA KWANZA : Alhamisi 4th June Kituo: St. John Maiella + St. Ann- Ngondi
Kwa jina la Baba na la Mwana, na la Roho Mtakatifu...
Ee Mtakatifu Antonio wa Padua, mnyenyekevu kwa watakatifu, upendo wako kwa Mungu na ukarimu duniani ilikustahilisha hapa duniani kupewa nguvu za miujiza. Miujiza mingi ilifanyika kwa nguvu za Kristu kupitia kwako, na wengi walisubiri kwa neno hilo ambalo ulikuwa tayari kusema.
Tukitumainia haya, twaomba utujalie neema tuombao kwa Mungu kupitia novena hii ( taja nia ). Majibu ya sala zetu twaamini zitafanyika kwa miujiza maana wewe pia ni mtakatifu wa miujiza. Ee Mnyenyekevu na mpendevu mtakatifu Antonio wa Padua, roho yako ilijawa na huruma kwa ulimwengu, tunakuomba ukaribishe sala zetu kwa Mtoto Yesu aliyependa kukaa mikononi mwako, na mwisho furaha ya mioyo yetu iwe kwako, kwa Kristu Bwana wetu...Amina
Baba yetu...........Salamu Maria.......Atukuzwe Baba..... Mtakatifu Antonio......Utuombee
SIKU YA PILI: Ijumaa 5th June
Kituo: Mtakatifu Patrick + Our Lady Moindabi
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu...Amina
Ee mtenda miujiza Mtakatifu Antonio wa Padua, kumbuka kwamba, hakuna aliyeachwa bila usaidizi kwa maombezi yako. Tukijazwa na nguvu hii, tuna ujasiri kukimbilia ulinzi na maombezi yako ee rafiki wa Yesu, ee mhubiri wa huruma ya Mungu, usitazame unyonge wetu bali yafikishe maombi yetu katika kiti cha enzi cha Mungu, yatie nguvu kwa maombezi yako na utujalie neema tuombayo katika novena hii ( taja nia hapa ). Amina
Baba yetu....Salamu Maria....Atukuzwe Baba... Mtakatifu Antonio wa Padua...Utuombee
2
SIKU YA TATU: Jumamosi 6th June
Kituo: Mtakatifu Thomas + Mtakatifu Elizabeti
Ee Mtakatifu Antonio wa Padua, msafi, ambaye katika uadilifu wako ulijaliwa kwa neema ya Mtoto Yesu, kumshika katika mikono na rohoni mwako. Tunakuomba utujalie hili tukuombalo.
Ee mtukufu Antonio wa Padua, ulizaliwa chini ya ulinzi wa Maria Mtakatifu, na katika kupalizwa kwake mbinguni amekuwa kwetu mwombezi na kimbilio letu, tunakuomba utuombee neema tuiombayo katika novena hii ( taja nia hapa ). Tuombee ee Mtakatifu Antonio mfanyikazi mkuu na mtenda miujiza ili Mungu ayajibu maombi yetu. Amina
Baba yetu........Salamu Maria.....Atukuzwe...... Mtakatifu Antonio wa Padua.... Utuombee
SIKU YA NNE: Jumapili 7th June
Kituo: Mary Immaculate + Teresa Ndabibi
Baba yetu...Salamu Maria...Atukuzwe Baba... Mtakatifu Antonio wa Padua....Utuombee
SIKU YA TANO: Jumatatu 8th June
Kituo: Mary Immaculate + St. Mark
Kwa jina la Baba ,na la Mwana, na la Roho Mtakatifu...
Tunakusalimu na kukuheshimu, Ee msaidizi mwenye nguvu, Mt.Antonio wa Padua.
Ulimwengu wa Kikristo unakuelekea na kupata uzoefu wa huruma yako na msaada wa nguvu
katika mahitaji mengi, na mateso ambayo tumehamasisha katika haja yetu ya kutafuta
msaada wako. Twakuomba ili tupate jibu nzuri kwa ombi letu la neema tunalotafuta katika
novena hii (taja nia yako hapa). Ee Mtakatifu Antonio wa Padua, nakusihi, nipate neema
ambayo natamani kwa maombezi yako. Amina.
Tunakusalimu ee Mtakatifu Antonio wa Padua, msafi naPambo la utukufu wa Ukristo.
Tunakusalimu, Mtakatifu mkuu, kerubi wa hekima na upendo wa Mungu. Hakika twafurahi
kwa neema aliyokupa Mungu wetu. Kwa unyenyekevu na ujasiri Ninakuomba unisaidie,
kwani ninajua kwamba Mungu amekupa upendo na huruma, pamoja na nguvu. Ninakuuliza
kwa upendo ambao wewe huhisi kwa Yesu mtoto mchanga ilivyofanyika katika mikono
yako, mweleze sasa atupe neema tunayotafuta kupitia maombi yako katika novena hii (taja
nia yako hapa).
3
Baba yetu...Salamu Maria...Atukuzwe Baba... Mtakatifu Antonio wa Padua... Utuombee
SIKU YA SITA: Jumanne 9th June
Kituo: St. Catherine + St. Raphael
Kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu...
Ewe mtukufu Mtakatifu Antonio wa Padua, ulichaguliwa na Mungu kuhubiri neno lake.
Ulipokea kipaji cha kunena kwa ndimi na nguvu ya kufanya kazi ya miujiza kutoka kwa
Mungu. Ewe Mtakatifu Antonia mwenye heri, niombee nitimize wajibu wa Mungu kwa yote
ili nimpende nawe katika milele yote.
Ee Mtakatifu Antonio wa Padua mkarimu, nakuomba uniombee neema ninayotamani kupitia
novena hii ( taja nia yako hapa). Amina
Baba yetu...Salamu Maria...Atukuzwe Mungu... Mtakatifu Antonio wa Padua...Utuombee
SIKU YA SABA: Jumatano 10th June
Kituo:St. Kizito + St. Elizabeth
Kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu...
Baba yetu...Salamu Maria...Atukuzwe Baba... Mtakatifu Antonio wa Padua...Utuombee
Ee Mtakatifu Antonio wa Padua uliye maarufu na bingwa katika imani na miujiza mingi
iliyotendeka kwako. Naomba uniombee katiku ukuu wa Bwana Yesu neema ninazohitaji
kupitia novena hii ( taja nia yako hapa).
Ee Mtakatifu Antonio wa Padua, uliye makini kwa wote wakuombao, nipe msaada kwa
maombezi yako yenye nguvu. Amina.
4
SIKU YA NANE: Alhamisi 11th June
Kituo: St. Joseph & St. John Mirera
Kwa jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu...
Mtakatifu Antonio wa Padua, wewe umeonyesha mwenyewe nguvu katika maombezi yako,
hivyo zabuni na uonyeshe huruma kwa wale wanaokuheshimu na kuomba katika mateso na
dhiki. Nakuomba sana kwa unyenyekevu na kwa dhati kunichukua mimi chini ya ulinzi wako
katika mahitaji yangu ya sasa na kupata kwangu neema ninayoomba katika novena hii (taja
nia yako hapa).
Pendekeza ombi langu kwa malkia wa mbinguni mwenye rehema, ili aweze kusihi sababu
yangu pamoja nawe mbele ya kiti cha enzi cha Mwana wa Mungu. Amina
Baba yetu...Salamu Maria...Atukuzwe Baba... Mtakatifu Antonio wa Padua...Utuombee
SIKU YA TISA: Ijumaa 12th June Kituo: St. Anthony of Padua Dck
Mtakatifu Anthony, mtumishi wa Maria, utukufu wa Kanisa, tuombee kwa ajili ya Baba yetu Mtakatifu, Askofu wetu,Mapadre,Mashemasi, Waseminari,Watawa wa kike na wa kiume, na waalimu wa dini, ili kwamba, kwa njia ya juhudi zao za kumcha Mungu na kazi ya kitume,
wote wanaweza kuwa Umoja katika imani na kutoa utukufu zaidi kwa Bwana.
Mt. Antonio wa Padua Msaidizi wa wote wanaokuomba, niombee kwa Mungu mbele ya kiti
chake cha enzi ili nitunukiwe neema katika novena hii ( taja nia yako hapa). Amina.
Baba yetu...Salamu Maria...Atukuzwe Baba...
Mtakatifu Antonio wa Padua...Utuombee
SHEREHE NI JUMAMOSI 13th . MTAKATIFU ANTONIO WA PADUA
Na iruhusiwe kupigwa chapa: Rev.Fr. Jude
Ikatafsiriwa kwa Kiswahili na: Shemasi Samuel Nyonje katika: samnyonje.blogspot.com
Imenakiliwa kwa Kiingereza kwenye:
https://www.ewtn.com/catholicism/devotions/novena-to-st-anthony-of-padua-302
5
No comments:
Post a Comment